WALINICHOMA KISU MARA NNE
Naitwa Moza, ni msukuma wa Bariadi. Sawa , mwaka 2022 nilimaliza chuo DUCE nakumbuka wiki moja kabla sijamaliza mtihani wangu wa mwisho wa UE, nilipigiwa simu na shangazi yangu aishiye Iringa mjini kwamba nimalizapo mitihani niende iringa nikamtembelee. Nikaona ni vyema sana maana mara ya mwisho yeye kuja Bariadi ilikuwa kipindi niko sekondari. Iliniongezea ulazima wa kwenda maana shangazi pia alikuwa amefiwa na watoto wake watatu tena vifo vya kutatanisha. Hivyo mimi kwenda ilikuwa namna pia ya kumtia moyo. Miaka yote nilipokuwa nakua, kwenye familia yetu kulikuwa na migogoro kati ya ndugu upande wa baba na upande wa mama . Nilikuwa sielewi nini haswa kilitokea huko nyuma . Nilijaribu kumuuliza mama shida ni nini lakini mama alinisihi kupuuza tu maisha yaendelee. wiki moja baadae nilikuwa nimeshamaliza mambo yote ya chuo. Nilipanda bus mpaka Iringa. Baada ya kufika Iringa shangazi alikuwa ameshanijulisha kuwa atamwagiza dereva ambaye ni rafiki yake anifuate anipeleke hadi ...